Numbers 11:1-6

Moto Kutoka Kwa Bwana

1 aBasi watu wakalalamika kwa habari ya taabu zao masikioni mwa Bwana, naye alipowasikia, hasira yake ikawaka. Ndipo moto kutoka kwa Bwana ukawaka miongoni mwao na kuteketeza baadhi ya viunga vya kambi. 2 bWatu walipomlilia Musa, akamwomba Bwana, nao moto ukazimika. 3 cHivyo mahali pale pakaitwa Tabera,
Tabera maana yake Kunaungua.
kwa sababu moto kutoka kwa Bwana uliwaka miongoni mwao.

Kware Kutoka Kwa Bwana

4 eUmati wa watu wenye zogo waliokuwa miongoni mwao walitamani sana chakula kingine, Waisraeli wakaanza kulia tena na kusema, “Laiti tungekuwa na nyama tule! 5 fTunakumbuka wale samaki tuliokula huko Misri bila gharama, pia yale matango, matikitimaji, mboga, vitunguu, na vitunguu saumu. 6 gLakini sasa tumepoteza hamu ya chakula; hatuoni kitu kingine chochote isipokuwa hii mana!”

Copyright information for SwhKC